window.__reverb = {}; window.__reverb.__reverbLoadedPromise = new Promise((resolve, reject) => { window.__reverb.__resolveReverbLoaded = resolve; window.__reverb.__rejectReverbLoaded = reject; }); window.__reverb.__reverbTimeout = setTimeout(() => { window.__reverb.__rejectReverbLoaded(); }, 5000);

'Kama waliteswa waje washtaki' Polisi Tanzania wawaambia wanaharakati

Kamanda wa Polisi Kanda maalum ya Dar es salaam Jumanne Muliro ameiambia BBC kuwa wanaharakati kutoka Kenya na Uganda Boniface Mwangi na Agatha Atuhaire kama waliteswa basi waende kushtaki katika mamlaka husika.

Muhtasari

Moja kwa moja

Rashid Abdallah & Ambia Hirsi

  1. Asante kwa kuwa nasi siku ya leo, Alamsiki!

  2. 'Kama waliteswa waje washtaki' Polisi Tanzania wawaambia wanaharakati

    Jumanne Muliro

    Kamanda wa Polisi Kanda maalum ya Dar es salaam Jumanne Muliro ameiambia BBC kuwa wanaharakati kutoka Kenya na Uganda Boniface Mwangi na Agatha Atuhaire kama waliteswa basi waende kushtaki katika mamlaka husika.

    Muliro ameongeza pia madai yao ni ya kiuanaharakati na ni maoni yao.

    Wanaharakati hao walieza jinsi walivyoteswa na mamlka za polisi nchini Tanzania kabla ya kurudishwa katika nchi zao.

    "Kama wangekuwa hapa, ningewashirikisha, ningewauliza wanasema nini, wanamaanisha nini... Katika sheria, mambo hayo yanaitwa ushahidi wa tetesi au tetesi," Jumanne Muliro aliiambia BBC. Alisema wanapaswa kutoa taarifa kwa mamlaka kwa ajili ya uchunguzi.

  3. Mashambulizi dhidi ya raia ni uhalifu wa kivita, mkuu wa haki za binadamu wa UN aonya

    Volker Türk

    Chanzo cha picha, EPA

    Mashambulizi dhidi ya raia yanajumuisha uhalifu wa kivita, mkuu wa haki za binadamu wa Umoja wa Mataifa anasema, huku akitoa wito wa uchunguzi huru kuhusu mauaji karibu na vituo vya kusambaza misaada huko Gaza katika siku za hivi karibuni.

    Volker Türk anasema kwa siku tatu mfululizo watu wameuawa karibu na kituo cha usambazaji chakula kinachoungwa mkono na Marekani na Israel, akisema waliohusika lazima wawajibishwe.

    Mashambulizi dhidi ya "raia wanaojaribu kupata kiasi kidogo cha chakula cha msaada huko Gaza" "hayana fahamu", anasema katika taarifa yake, na kuongeza: "Mashambulizi yanayoelekezwa dhidi ya raia yanajumuisha uvunjaji mkubwa wa sheria za kimataifa, na uhalifu wa kivita." "Wapalestina wamekabiliwa na chaguo baya zaidi: kufa kutokana na njaa au hatari ya kuuawa wakati wakijaribu kupata chakula kidogo ambacho kinapatikana kupitia utaratibu kwa usaidizi wa kibinadamu wa kijeshi wa Israel," anasema.

    "Kizuizi cha makusudi" cha kupata misaada "kinaweza kuwa uhalifu wa kivita," Türk anasema.

    "Tishio la njaa, pamoja na miezi 20 ya mauaji ya raia na uharibifu kwa kiwango kikubwa, uhamisho wa mara kwa mara wa kulazimishwa, usiovumilika, maneno ya kudhalilisha utu na vitisho vya uongozi wa Israel kuondoa kanda wa wakazi wake, pia ni vipengele vya uhalifu mkubwa zaidi chini ya sheria za kimataifa," anasema.

  4. Wawili wafariki katika mlipuko Uganda

    Kila mwaka maelfu kwa maelfu ya mahujaji na watalii hufika katika eneo la Namugongo kwa ajili ya maadhinisho ya mashahidi wa Uganda

    Chanzo cha picha, Uganda Martyrs Shrine/Facebook

    Maelezo ya picha, Kila mwaka maelfu kwa maelfu ya mahujaji na watalii hufika katika eneo la Namugongo kwa ajili ya maadhinisho ya mashahidi wa Uganda

    Watu wawili wamefariki baada ya mlipuko kutokea katika mji mkuu wa Uganda Kampala wakati nchi hiyo inaadhimisha Siku ya Mashahidi wa Kikristo.

    Tukio hilo lilitokea karibu na moja ya makaburi ambapo maelfu ya waumini wa Kikristo walikuwa wamekusanyika.

    Kulingana na vyombo vya habari vya ndani, waathiriwa ni mwanamume na mwanamke waliokuwa wakiendesha pikipiki.

    Hata hivyo, Chris Magezi, msemaji wa muda wa jeshi hilo amedai waliofariki ni magaidi ambao walikamatwa wakiwa na vilipuzi.

    Usalama umeimarishwa katika eneo la tukio. Hata hivyo mamilioni ya mahujaji wamemiminika mjini Namugongo kusherehekea Siku kuu ya Mashahidi wa Kikristo.

    Tukio hilo ambalo ni mojawapo ya mahujaji wengi zaidi wa Kikristo barani Afrika, huwavutia mamilioni ya waumini kila mwaka kuwaenzi mashahidi 45 wa Uganda, Wakatoliki 22 na Waanglikana 23 waliouawa kati ya mwaka 1885 na 1887 kwa amri ya Kabaka Mwanga II wa Buganda kwa kukataa kuacha imani yao.

    Nchini Uganda, Juni 3 ni sikukuu ya umma, na maelfu ya watu wanaanza safari ya hija kwa miguu.

  5. Uingereza yatishia kumshitaki Abramovich - Kunani?

    ,

    Chanzo cha picha, UEFA via Getty Images

    Serikali ya Uingereza imetishia kumshtaki mmiliki wa zamani wa Klabu ya Soka ya Chelsea Roman Abramovich ili kushinikiza fedha zitakazotokana na mauzo ya klabu hiyo zinawafaidi raia wa Ukraine.

    Mapato ya takriban pauni bilioni 2.5 yamezuiliwa katika akaunti ya benki ya Uingereza tangu kuuzwa kwa klabu hiyo, baada ya Bw Abramovich kuwekewa vikwazo kufuatia uvamizi wa Urusi nchini Ukraine mnamo Februari 2022.

    Serikali ya Uingereza inataka pesa hizo zitolewa kwa mashirika ya misaada ya kibinadamu ya Ukraine, lakini Bw Abramovich anataka ziende kwa "waathiriwa wote wa vita nchini Ukraine".

    Katika taarifa ya pamoja, Kansela Rachel Reeves na Waziri wa Mambo ya Nje David Lammy walisema: "Mlango wa mazungumzo utaendelea kuwa wazi, tuko tayari kufuatilia hili kupitia mfumo wa mahakama tukuhitajika kufanya hivyo."

    Soma pia:

  6. Polisi Tanzania wazingira kanisa la Askofu Gwajima

    Askofu Gwajima

    Chanzo cha picha, GWAJIMA FACEBOOK

    Polisi jijini Dar es Salaam Tanzania wameripotiwa kulizingira eneo lilipo jengo la kanisa la Ufufuo na Uzima linalomilikiwa na kiongozi wa dini ambaye pia ni Mbunge wa Kawe, Josephat Gwajima.

    Hatua hiyo ilikuja saa chache baada ya kusambaa mtandaoni barua kutoka moja ya idara za Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi ya Tanzania ikimuarifu Gwajima kuhusu uamuzi wa serikali kulifunga kanisa hilo.

    Taarifa za askari polisi kulizingira jengo la kanisa la Ufufuo na Uzima lililopo eneo la Ubungo, kilomita 12 kutoka katikati mwa Dar es Salaam zilisambazwa mtandaoni na Gwajima mwenyewe kupitia kipande cha picha ya video akiwa amezungukwa na watu aliowaita maaskofu wa kanisa hilo waliovalia makoti na mashati ya rangi ya zambarau.

    Baadaye zilisambaa picha zilizowaonesha watu wakirusha mawe na sauti za kuwahimiza waumini kwenda kanisani huku kukiwa na milio ambayo haikufahamika iwapo ilikuwa ni ya gesi ya kutoa machozi au risasi za moto.

    Barua ya msajili wa jumuiya za kiraia iliyosambaa ambayo Gwajima anasema hajaipookea, ilielezea kufuta usajili wa kanisa la Glory of Christ Church maarufu Ufufuo na Uzima hivyo kutakiwa kusitisha shughuli zote mara moja kwa makosa ya kutoa mahubiri yanye mwelekeo wa kisiasa na kuichonganisha serikali na wananchi.

    Mapema Mei 25 Gwajima alielezea kukerwa na matendo ya utekaji wa watu na mauaji.

    Maelezo zaidi:

  7. Hujambo na karibu

    Nikukaribishe katika taarifa zetu za moja kwa moja, leo Jumanne ya tarehe 3 Juni 2025