Presha 6 zinazoikabili Simba SC dhidi ya Berkane Zanzibar

S

Chanzo cha picha, Getty Images

  • Author, Yusuph Mazimu
  • Nafasi,
  • Akiripoti kutoka Dar es Salaaam

Simba SC inakaribia kucheza moja ya mechi zake kubwa zaidi katika historia ya klabu hiyo, mchezo wa marudiano wa fainali ya Kombe la Shirikisho Afrika dhidi ya Renaissance Sportive de Berkane ya Morocco (RS Berkane) Jumapili hii.

Baada ya kupoteza kwa mabao 2-0 ugenini kwenye dimba la Berkane, Wekundu hao wa Msimbazi wanahitaji ushindi wa angalau mabao 3-0 ili kugeuza matokeo na kutwaa taji lao la kwanza barani Afrika.

Kocha wa Simba Fadlu Davids anasema; "Tulifungwa mabao mawili ya mapema ambayo yalituzuia, lakini nina matumaini tunaweza bado kufanya vizuri zaidi katika mchezo wa marudiano."

Katika kipindi ambacho mashabiki wa klabu hiyo wamejaa matumaini na msisimko, pia kuna hali ya wasiwasi na presha kubwa inayoizunguka timu hiyo na hasa presha hizi sita.

1. Presha ya kupindua matokeo ya Morocco

S

Chanzo cha picha, CAF

Maelezo ya picha, Berkane inakwenda Zanzibar ikiwa na faida ya mabao 2-0 iliyoyapata Morocco katika mchezo wa kwanza

Simba wanakabiliwa na mlima mrefu kufuta mabao mawili ya ugenini dhidi ya timu ngumu ya Berkane. Katika hatua ya makundi, Berkane walifungwa mechi moja tu kati ya sita, na walionesha uimara wa kujilinda. Hakuna mechi waliyopoteza kwa mabao mawili na zaidi. Kwa Simba, hilo lina maana kuwa lazima wachanganye akili zao, za kuambiwa, nidhamu, ubunifu na kasi ya mashambulizi.

Skip Iliyosomwa zaidi and continue reading
Iliyosomwa zaidi