Ukraine iliachana na silaha zake za nyuklia. Lakini sasa inauliza kwanini ilifanya hivyo

Oleksandr sasa anasimamia jumba la makumbusho ambapo silaha za nyuklia zilihifadhiwa

Chanzo cha picha, BBC/Kostas Kallergis

Chini ya wingu zito la kijivu na kutanda kwa theluji, mabaki ya kijivu na kijani ya Vita baridi yanakumbusha siku zilizoshuhudiwa hapo nyuma nchini Ukraine.

Makombora, na silaha nzito za kivita vimesalia kama ukumbusho wa enzi ambazo Ukraine ilikuwa na jukumu muhimu katika mpango wa silaha za kinyuklia katika muungano wa Kisoviet.

Hata hivyo makombora hayo ya asili, yana nyufa na kujaa vumbi.

Kwa zaidi ya miaka 30 handaki hilo limejaa vumbi.

Ngome nzima, karibu na jiji la Pervomais’k katikati mwa Ukraine, limegeuka kuwa jumba la makumbusho kwa muda mrefu.

Ukraine mpya ilipoibuka kutoka chini ya kivuli cha Moscow mwanzoni mwa miaka ya 1990, Kyiv ilikataa silaha za nyuklia.

Lakini karibu miaka mitatu baada ya uvamizi kamili wa Urusi, na bila makubaliano ya wazi kati ya washirika kuhusu jinsi ya kudhamini usalama wa Ukraine vita vitakapomalizika, wengi sasa wanahisi hilo lilikuwa kosa.

Takriban miaka 30 iliyopita, mnamo 5 December 1994 katika maadhimisho ya Budapest, Ukraine iliungana na Belarus na Kazakhstan katika kuachana na silaha za kinyuklia kama hatua ya kuhakikisha usalama kutoka Marekani, Uingereza, Ufaransa, Uchina na Urusi.

Kwa msisitizo, makombora yalikuwa ni ya muungano wa Kisoviet si ya jamhuri za zamani.

Lakini theluthi moja ya hifadhi ya nyuklia ya USSR ilikuwa kwenye ardhi ya Ukraine na kukabidhi silaha kulizingatiwa kama wakati muhimu, unaostahili kutambuliwa kimataifa.

"Ahadi juu ya uhakikisho wa usalama ambao [tume]toa mataifa haya matatu...tunasisitiza kujitolea kwetu kwa uhuru, mamlaka na uadilifu wa eneo la mataifa haya," Rais wa Marekani wakati huo Bill Clinton alisema huko Budapest.

Akiwa kijana aliyehitimu katika chuo cha kijeshi huko Kharkiv, Oleksandr Sushchenko aliwasili Pervomais'k miaka miwili baadaye, mchakato wa kumvua uanachama ulipokuwa ukiendelea.

Alitazama jinsi makombora yalivyokuwa yakitolewa na kusafishwa.

Sasa amerejea kama mmoja wa wasimamizi wa jumba la makumbusho.

Oleksandr anafikiri Ukraine isingeachana na silaha zake za kinyuklia.

Chanzo cha picha, BBC/Kostas Kallergis

Akiangalia nyuma baada ya miaka kumi ya taabu iliyosababishwa na Urusi, ambayo jumuiya ya kimataifa imeonekana kushindwa au kutotaka kuzuia, hufikiria hatma isiyoepukika.

Nikishuhudia kinachoendelea Ukraine sasa, mtazamo wangu ni kwamba ilikuwa kosa kubwa kuteketeza kabisa silaha za nyuklia'', anasema

''Hata hivyo ilikuwa ni suala la kisiasa''. Uamuzi ulifanywa na uongozi wa juu na sisi tulitekeleza tu''.

Wakati huo ulionekana kuwa sawa. Hakuna aliyefikiria kwamba Urusi ingeishambulia Ukraine ndani ya miaka 20.

"Hatukufahamu vizuri lakini pia tuliamini," alisema Serhiy Komisarenko, ambaye alikuwa akihudumu kama balozi wa Ukraine huko London mwaka wa 1994.

Wakati Uingereza na Marekani na baadaye Ufaransa ikajiunga ''anasema tulikuwa tunafikiri imetoka, unajua, na Urusi pia.

Kwa nchi masikini kuibuka tu kutoka kwenye miongo ya utawala wa Kisoviet, wazo la kuendeleza mradi ghali wa silaha za nyuklia haukuonekana wa maana sana.

"Kwa nini utumie pesa kutengeneza silaha za nyuklia au kuzihifadhi," Komisarenko asema, "ikiwa unaweza kuzitumia kwa viwanda, kwa maendeleo");